Wakati ni sasa kwetu si wakenya
Kuwafunza wanasiasa kuwa tumeshamanya
Hila zao za ufala hawataweza kutukanganya
Kura yetu ndio kiboko yao.
Juzi wasubiri usiku ati kujipa mamilioni
"Leo nawaita mafi ya kuku mnafikiria hatuoni"
Ufisadi mwafanya usiku wakenya wafa hospitalini
Kura yetu ndio kiboko yao
Nawaambia ukweli hawa nyie wabunge mafidhuli
Tumeishaipata yenu dawa fedha zetu tena hamli
Tunawachukia kama chawa hatuwapi tena shughuli
Kura ndio kiboko yao.
Nawasihi wote wakenya tujitokeze kwa wingi
Tariki ni nne machi tuwaonyeshe mwenye nguvu
Kwa umoja na udugu tutende haki yetu
Kura yetu ndio kiboko yao.
Comments
Post a Comment