Skip to main content

Mambo Ya Badilika:




Tariki yenyewe nane nane,  imewadia
Wakati sasa ni wetu, wananchi kujitetea
Hakikisha kura umepiga kwa asiye na doa
Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika

Siasa duni za ufidhuli kataa katakata
Walowezi na wafisadi tupa kama taka
Kamwe hatutaki damu tena kumwagika
Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika

Wito natoa, kwetu sisi vijana
Kesho hatofika, uongozi tungechukua jana
Wazee twawaeleza na tena kwa bayana
Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika

Mamlaka msipo tupa hatuna budi kuyanyakua  
Miaka mingi ya ujana tumepoteza kiholela
Kwa kutumiwa vibaya na wakorofi wanasiasa
Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika







Comments

Popular posts from this blog

Umuhimu wa kiswahili

Kiswahili ni mojawapo wa lugha za kiafrika ambayo inakua kwa kasi mno. Katika Afrika ya mashariki kiiswahili knazungumzwa kati nchi za Kenya, Tanzania ,Uganda, Rwanda na Burundi. Aidha kiswahili kinazungumzwa katika nchi za Congo na Zaire. Hapa nchini kenya na Tanzania kiswahili kimefanywa kuwa lugha rasmi hali kadhalika lugha ya taifa. kiswahili pia kimefanywa kuwa lugha rasmi katika kongamano zote za Umajo wa Afrika yaaani African Union.  Hivyo basi tukizingatia haya hatuna budi kusema ya kwamba nafasi na manufaa ya kiswahili katika lugha ya kiswahili ni chungu nzima. Katika makala haya yetu tutazidi kuangazia lugha ya kiswahili kama kigezo cha undeleshaji wa uchumi barani Afrika na ulimwenguni kote kwa ujumla.