Skip to main content

Posts

Mambo Ya Badilika:

Tariki yenyewe nane nane ,  imewadia Wakati sasa ni wetu, wananchi kujitetea Hakikisha kura umepiga kwa asiye na doa Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika Siasa duni za ufidhuli kataa katakata Walowezi na wafisadi tupa kama taka Kamwe hatutaki damu tena kumwagika Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika Wito natoa, kwetu sisi vijana Kesho hatofika, uongozi tungechukua jana Wazee twawaeleza na tena kwa bayana Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika Mamlaka msipo tupa hatuna budi kuyanyakua   Miaka mingi ya ujana tumepoteza kiholela Kwa kutumiwa vibaya na wakorofi wanasiasa Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika
Recent posts

KURA YETU, KIBOKO YAO

Wakati ni sasa kwetu si wakenya Kuwafunza wanasiasa kuwa tumeshamanya Hila zao za ufala hawataweza kutukanganya Kura yetu ndio kiboko yao. Juzi wasubiri usiku ati kujipa mamilioni "Leo nawaita mafi ya kuku mnafikiria hatuoni" Ufisadi mwafanya usiku wakenya wafa hospitalini Kura yetu ndio kiboko yao Nawaambia ukweli hawa nyie wabunge mafidhuli Tumeishaipata yenu dawa fedha zetu tena hamli Tunawachukia kama chawa hatuwapi tena shughuli Kura ndio kiboko yao. Nawasihi wote wakenya tujitokeze kwa wingi Tariki ni nne machi tuwaonyeshe mwenye nguvu Kwa umoja na udugu tutende haki yetu Kura yetu ndio kiboko yao.

Kiswahili Kitukuzwe

Ubeti wa kwanza natoa wito Kwa wakenya wapendwa Lugha ndiyo kiini cha mazungumzo Huleta watu pamoja Huwa kiwakilishi cha jamii Kiswahili lugha ya taifa Kinatumika hata ughaibuni Wenyaji twakipuuza Tukienzi kiingereza Ukoloni mamboleo Kila siku twaendeleza Kiaswahili twakidhihaki Utamaduni wetu twautupa Mwacha mila ni mtumwa Ndio maana twaangaika Hatujui lipi la kufuata Uingereza ama Marekani Nawasihi wapendwa Fikra tuzindue Tufuate yetu Waafrika Tujiendeleze ipasavyo Kiswahili tukikuze Tujivunie lugha yetu

Umuhimu wa kiswahili

Kiswahili ni mojawapo wa lugha za kiafrika ambayo inakua kwa kasi mno. Katika Afrika ya mashariki kiiswahili knazungumzwa kati nchi za Kenya, Tanzania ,Uganda, Rwanda na Burundi. Aidha kiswahili kinazungumzwa katika nchi za Congo na Zaire. Hapa nchini kenya na Tanzania kiswahili kimefanywa kuwa lugha rasmi hali kadhalika lugha ya taifa. kiswahili pia kimefanywa kuwa lugha rasmi katika kongamano zote za Umajo wa Afrika yaaani African Union.  Hivyo basi tukizingatia haya hatuna budi kusema ya kwamba nafasi na manufaa ya kiswahili katika lugha ya kiswahili ni chungu nzima. Katika makala haya yetu tutazidi kuangazia lugha ya kiswahili kama kigezo cha undeleshaji wa uchumi barani Afrika na ulimwenguni kote kwa ujumla.