Skip to main content

Kiswahili Kitukuzwe

Ubeti wa kwanza natoa wito
Kwa wakenya wapendwa
Lugha ndiyo kiini cha mazungumzo
Huleta watu pamoja
Huwa kiwakilishi cha jamii
Kiswahili lugha ya taifa
Kinatumika hata ughaibuni
Wenyaji twakipuuza
Tukienzi kiingereza
Ukoloni mamboleo
Kila siku twaendeleza
Kiaswahili twakidhihaki
Utamaduni wetu twautupa
Mwacha mila ni mtumwa
Ndio maana twaangaika
Hatujui lipi la kufuata
Uingereza ama Marekani
Nawasihi wapendwa
Fikra tuzindue
Tufuate yetu Waafrika
Tujiendeleze ipasavyo
Kiswahili tukikuze
Tujivunie lugha yetu




Comments

Popular posts from this blog

Umuhimu wa kiswahili

Kiswahili ni mojawapo wa lugha za kiafrika ambayo inakua kwa kasi mno. Katika Afrika ya mashariki kiiswahili knazungumzwa kati nchi za Kenya, Tanzania ,Uganda, Rwanda na Burundi. Aidha kiswahili kinazungumzwa katika nchi za Congo na Zaire. Hapa nchini kenya na Tanzania kiswahili kimefanywa kuwa lugha rasmi hali kadhalika lugha ya taifa. kiswahili pia kimefanywa kuwa lugha rasmi katika kongamano zote za Umajo wa Afrika yaaani African Union.  Hivyo basi tukizingatia haya hatuna budi kusema ya kwamba nafasi na manufaa ya kiswahili katika lugha ya kiswahili ni chungu nzima. Katika makala haya yetu tutazidi kuangazia lugha ya kiswahili kama kigezo cha undeleshaji wa uchumi barani Afrika na ulimwenguni kote kwa ujumla.

Mambo Ya Badilika:

Tariki yenyewe nane nane ,  imewadia Wakati sasa ni wetu, wananchi kujitetea Hakikisha kura umepiga kwa asiye na doa Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika Siasa duni za ufidhuli kataa katakata Walowezi na wafisadi tupa kama taka Kamwe hatutaki damu tena kumwagika Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika Wito natoa, kwetu sisi vijana Kesho hatofika, uongozi tungechukua jana Wazee twawaeleza na tena kwa bayana Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika Mamlaka msipo tupa hatuna budi kuyanyakua   Miaka mingi ya ujana tumepoteza kiholela Kwa kutumiwa vibaya na wakorofi wanasiasa Haijalishi NASA au Jubilee mambo yabadilika